Beki wa Real Madrid Dani Carvajaal amefunga goli dakika ya 119 dhidi ya sekatika dakika za nyongeza na kifanya Real Madrid kuibuka na ushindi wa mabao matatu kwa mawili.
Baada ya kumalizika kwa mechi ya ngao ya jamii iliyomalizika kwa manchester united kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya leicester kocha wa timu hiyo ya Old Traford Jose Mourinho amethibitisha kua Paul Pogba ni mchezaji wa United baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Juventus.
Kuna mgongano wa mawazo wa hali ya juu kati ya kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane na Rais wa timu hiyo Florentino Perez Juu ya kiungo yupi wa kusajili.
Member wa bodi ya FIFPro Dejan Stefanovic amesema kitendo cha Mourinho kumwambia Bastian Schweinsteiger kufanya mazoezi na wachezaji wa akiba si cha kiungwana na ingekua ni katika medali nyingine tofauti na soka kocha huyo angepigwa miaka mitau jela kwa kufananisha kitendo hicho na unyanyasaji wa hali ya juu.
Beki wa kushoto wa Brazil na Real Madrid Marcelo amesema uwezo wa Zidane kama kocha ni wa hali ya juu baada ya kocha huyo kufanya makubwa katika kipindi kidogo alichokaa clabuni hapo. Zidane anaekalia kiti cha moto baada ya kumrithi kocha aliyetimuliwa clubuni hapo rafa Benitez alishinda mechi 17 kati ya 20 zilizokua zimesalia kumaliza ligi na kuifanya Barcelona kua katika presha ya hali ya juu baada ya kuipumulia kwa karibu sana club hiyo ya Katalunya hadi mwisho wa ligi.
Mchezaji wa zamani wa club ya PSG aliyetua msimu huu katika mji wa Manchester kukipiga katika club ya Man U Zlatan Ibrahimovich amenena kua uamuzi wake wa kutua United kuungana na kocha wake wa zamani mreno Jose Mourinho sio jambo la kupoteza muda bali kushinda vikombe.
Mabingwa mara tano wa dunia Brazil jana wametupwa nje ya mashindano ya Copa America 2016 yanayofanyika pale USA.
Timu hiyo iliyo chini ya kocha Dunga imeendelea kuleta aibu kwa wabrazil kwa mara nyingine tena baada ya kuchapwa na timu dhaifu ya Peru isiyo na wachezaji wazoefu katika ngazi ya kimataifa tofauti na brazil ilikua na wachezaji kama Willian, Miranda, Coutinho na wengineo.